Mshonaji wa Bidhaa za Ngozi

Advertisement      

Mshonaji wa Bidhaa za Ngozi

Mon Apr 02, 2018

Job Role: Entry Level Position Type: Full Time Organization Type: Private Sector Location: Ilala, Ilala Dar Es Salaam Description MAJUKUMU YA KAZI i. Kufanya kazi kwa vitendo katika fani ya ushonaji na uundaji wa bidhaa za ngozi ii. Kubuni na Kutengeneza bidhaa tofauti tofauti za Ngozi. SIFA ZA MWOMBAJI 1. Awe amepitia mafunzo ya ushonaji wa bidhaa za ngozi ya chuo kinachotambulika. 2. Awe na ujuzi mzuri wa kushona bidhaa za ngozi. 3. Awe na mifano ya bidhaa ambazo amewahi kuzitengeneza. 4. Awe m'bunifu mwenye uwezo wa kutengeneza bidhaa zenye viwango vya juu. 5. Awe mwenye uwezo wa kusimamia muda na kukamilisha kazi kwa muda uliopangwa. 6. Aweze kubadilika kulingana na mazingira na kukidhi mahitaji ya wateja. 7. Awe na hamasa na kazi anazozifanya pasipo usimamizi. 8. Awe mwaminifu na utii katika kazi. 9. Awe mwenye uwezo mzuri wa kuzungumza na ushawishi kwa wateja MASHARITI YA MAOMBI YA KAZI i. Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania na wenye umri usiozidi miaka 45 ii. Waombaji waambatishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed C.V) yenye anwani na namba za simu za kuaminika pamoja na majina ya wadhamini (referees) wawili wa kuaminika. iii. Maombi yote yaambatane na vyeti vya taaluma, maelezo, nakala za vyeti vya na vyeti vya kuhitimu mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika. iv. Uwasilishaji wa taarifa na sifa za kugushi wahusika watachukuliwa hatua za kisheria. v. Mwisho wa kutuma maombi ya kazi ni tarehe 15 Aprili, 2018. vi. Maombi yatakayowasilishwa nje ya utaratibu ulioainishwa katika tangazo hili HAYATAFIKIRIWA vii. Maombi yote yatumwe kwenye barua pepe brimaenterprise@gmail.com MUHIMU: KUMBUKA KUAMBATISHA BARUA YAKO YA MAOMBI YA KAZI.

Write Your Comments

Reviews

copyrights © 2024 123Tanzania.com   All rights reserved. Designed & Maintained by Powerweb